Boda boda Mbili zikiwa zimegongana
VONCE PRINCE
Jumatano, 1 Januari 2014
Jumatano, 11 Septemba 2013
NDUNGAI NA MBOWE WALIVUNJA KANUNI ZA BUNGE MAKUSUDI KWA MASLAHI YA VYAMA VYAO
Kumekuwa na mjadala mkali kuhusu iwapo Naibu Spika, Job Ndugai alikiuka Kanuni za Bunge katika kushughulikia vurugu zilizotokea Bungeni Alhamisi iliyopita kwa kuamuru kutolewa nje kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.
Ndugai ambaye alikuwa kiongozi wa shughuli za Bunge siku hiyo, aliwaamuru askari kumtoa nje Mbowe baada ya kukaidi amri yake ya kutaka kuketi chini aliposimama kutaka kupewa nafasi ya kuzungumza, hali iliyozua tafrani bungeni.
Pamoja na mambo mengine Ndugai amekuwa akituhumiwa kwamba anaminya uhuru wa wabunge wa upinzani kutokana na mapenzi aliyonayo kwa chama chake, CCM.
Kwa upande mwingine, kumekuwa na lawama kwamba Mbowe alikosea kukaidi amri ya Naibu Spika kwa kuwa kanuni zinamtaka mbunge yeyote (hata akiwa waziri), kuketi pale kiongozi wa Bunge (Spika, Naibu au Mwenyekiti) anaposimama, hivyo kusababisha mtafaruku.
Mwenyekiti wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, Profesa Chris Peter Maina alisema tatizo lililojitokeza bungeni linaweza kumalizwa na kuwapo kwa sheria inayokataza Spika wa Bunge kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa.
“Unajua kwa Katiba ya sasa Spika wa Bunge anaweza kuwa mwadilifu lakini akapata shinikizo kutoka upande wa chama chake, Ibara ya 128 ya Rasimu ya Katiba Mpya inaeleza kiundani kuhusu spika kutokutoka miongoni mwa wabunge jambo ambalo ni zuri,” alisema Profesa Maina na kuongeza:
“Mwenendo wa Bunge siyo mzuri. Wabunge hawaheshimiani hata kidogo, nadhani wanahitaji kukubaliana kwa hoja, wao ndiyo wanatunga sheria, hivyo wanatakiwa kulumbana kwa kufuata utaratibu uliowekwa.”
Spika wa zamani, Pius Msekwa alisema wakati akiongoza Bunge hakuwahi kuona vurugu, fujo na malumbano ya wabunge kama ilivyotokea Alhamisi iliyopita.
“Wakati nikiwa Spika sikumbuki kama kuna siku ziliwahi kutokea vurugu za aina hii, kilichotokea ni sawa na uhalifu kwa sababu taratibu hazikufuatwa,” alisema Msekwa.
Matakwa ya Kanuni
Ibara ya 76 (1) na (2) ya Kanuni za Bunge Toleo la Aprili 2013, zinaeleza jinsi ya kudhibiti fujo bungeni, lakini Ndugai anakosolewa kwamba hakuzingatia taratibu hizo kushughulikia vurugu za Alhamisi.
Kanuni ya 76 (1) inasema: “Kwa madhumuni ya kudhibiti fujo endapo itatokea ndani ya Ukumbi wa Bunge na Spika ataona kuwa kuna haja ya kutumia nguvu, basi anaweza kuahirisha shughuli za Bunge bila ya hoja yoyote kutolewa au kusitisha kikao kwa muda atakaoutaja ili fujo hiyo iweze kudhibitiwa na Mpambe wa Bunge”.
Kadhalika, fasili ya pili ya Kanuni hiyo inasema: “Baada ya utulivu kurudia, Spika atalipeleka kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge suala ambalo lilisababisha kutokea kwa fujo ikiwa ni pamoja na jina la mbunge au majina ya wabunge waliohusika na fujo hiyo ili kamati hiyo iweze kulishauri Bunge kuhusu adhabu inayostahili kutolewa”.
Wakati vurugu zilipozuka bungeni, Ndugai aliwaita askari badala ya mpambe, kumtoa nje Mbowe na hakuwa amesitisha wala kuahirisha shughuli za Bunge kama kanuni zinavyotaka.
Pia Naibu Spika alitangaza kumsamehe Mbowe na Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ kwa maana ya kuwaruhusu kuendelea na vikao vya Bunge siku hiyo jioni, badala ya suala hilo kupelekwa kwenye kamati husika kama kanuni ya 76 (2) inavyoelekeza.
Utetezi wa Ndugai
Ndugai alisema hakuzingatia kanuni hizo kwani mazingira ya vurugu hizo hayaendani na kanuni husika, hivyo alitumia nafasi yake ambayo pia inatambuliwa na kanuni za Bunge.
“Vurugu zilikuwa zimepangwa na zilifanywa kwa makusudi ili kuhakikisha kwamba shughuli za Bunge zinakwama maana hiyo kanuni wanafahamu kwamba ipo, sasa hatuwezi kuwa na Bunge ambalo mtu akiamua tu anafanya fujo ili liahirishwe,” alisema Ndugai na kuongeza:
“Mimi kama kiongozi wa shughuli za siku hiyo, kazi yangu ni kuhakikisha kwamba shughuli zilizopangwa zinafanyika, kwa hiyo nisingeweza kuruhusu watu wachache watukwamishe kutokana na masilahi yao.”
Alipoulizwa kwamba alifahamu vipi kuwapo kwa njama hizo, alisema kauli na matendo ya wabunge wa upinzani vilionekana tangu mwanzo wa mjadala kutaka kukwamisha shughuli za Bunge siku hiyo.
Kuhusu kuwatangazia wabunge hao msamaha badala ya kupeleka suala hilo kwenye kamati husika, Ndugai alisema: “Hakukuwa na adhabu kubwa ya kuwapa zaidi ya kuwatangazia msamaha.”
“Niliwasamehe kwa mujibu wa kanuni maana zinaruhusu kuzingatia uamuzi ambao uliwahi kutolewa na maspika waliopita, kwa hiyo kama unakumbuka kesi ya Mengi (Regnald) na Malima (Adam), Spika Samuel Sitta baada ya kumwita Malima akakataa kwenda alisema anamsamehe,” alisema na kuongeza:
“Yeye (Sitta) alitumia neno kwamba nimeamua kumpuuza lakini mimi sikusema hivyo, nilisema kwamba namsamehe kwa sababu tu namheshimu na ni kiongozi mkubwa tu katika jamii”.
Lissu amtetea Mbowe
Mbowe hakupatikana juzi na jana kuzungumzia suala hilo, lakini Mnadhimu Mkuu wa Upinzani Bungeni, Tundu Lissu alisema kiongozi wake huyo hakufanya makosa kwani alisimama wakati Mbunge wa Vunjo (TLP), Augustine Mrema alipokuwa akizungumza na kwamba hilo siyo kosa kikanuni.
Alisema Ndugai alipaswa kumheshimu Mbowe kwa kuzingatia wadhifa wake bungeni na kwamba kitendo cha kumwambia “kaa chini” hakikubaliki.
“Hatuwezi kuruhusu na hatutaruhusu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kudhalilishwa, ikiwa tutaruhusu hilo litokee, basi miongoni mwetu sisi wapinzani hakuna atakayepona,” alisema Lissu na kuongeza:
“Naibu Spika amelidhalilisha Bunge kwa sababu kwa kumdharau Mbowe ni kwamba amemdharau mmoja wa viongozi wakuu wa Bunge”.
-Mwananchi
KILICHOMUUA MSANII HUYU KINASIKITISHA.....!!!
TASNIA ya filamu Bongo imepata pigo lingine baada ya mwishoni mwa wiki iliyopita kuondokewa na msanii aliyekuwa akichipukia kwa kasi aliyefahamika kwa jina la Zuhura Maftah ‘Malisa’.
Malisa alifariki dunia katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar baada ya kusumbuliwa na uvimbe kichwani kwa takriban miezi mitatu.
Wakizungumza na gazeti hili mara baada ya kifo hicho, baadhi ya wasanii wa filamu walielezea masikitiko yao na kusema hakika wamemkosa msanii ambaye siku za baadaye angekuwa moto wa kuotea mbali.
“Kifo chake kimetusikitisha sana, Malisa alikuwa mmoja wa wasanii ambao walikuwa wakija kwa kasi, amefariki dunia wakati ndiyo kwanza nyota yake ilikuwa imeanza kung’ara lakini kazi ya Mungu siku zote haina makosa, akapumzike kwa amani,” alisema mmoja wasanii aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Msanii mwingine wa filamu ambaye huenda kifo hicho kimemgusa kuliko wengine ni Yvonne Cheryl ‘Monalisa’ ambaye inadaiwa muda mfupi kabla ya Malisa kufariki waliongea na kumwambia anaendelea vizuri.
Mmoja wa watu waliokuwa wakimhudumia Malisa hospitalini hapo aliyefahamika kwa jina la Vanitha alisema: “Siku ya kifo chake aliniambia nimpigie simu Mona aongee naye kwani hajamuona siku hiyo, ilikuwa saa 12 jioni baada ya kumaliza kumuogesha.
“Waliongea na kumwambia anaendelea vizuri. Baada ya Malisa kumaliza kuongea na Mona niliondoka lakini nilipofika Surender Bridge nikapata taarifa kuwa amefariki dunia,” alisema Vanitha.
Mtoto mwenye miaka 8 afariki kutokana na majeraha ya ngono usiku wa harusi yake akiwa na mume wake alie na mara tano ya umri wake
Bibi harusi mtoto mwenye umri wa mika 8 amefariki dunia usiku wa harusi yake baada ya mateso ya majeraha ya ndani kutokana na kiwewe ngono (Sexual trauma).
Kifo kilitokea katika eneo la kikabila la Hardh kaskazini magharibi mwa Yemen, ikipakana na Saudi Arabia.
Haki za binadamu imeshatoa wito kwa kukamatwa kwa mume wake ambaye alikuwa mara tano ya umri wa mtoto huyo.habari hii imeleta attention zaidi kutokana na kuwepo kwa ndoa za kulazimishwa kwa watoto katika kanda ya mashariki ya kati.
"Kutokana na Umoja wa Mataifa ya Idadi ya Watu (UNFPA), kati ya 2011 na 2020, zaidi ya wasichana milioni 140 watakuwa wanaharusi watoto, Aidha katika wasichana hao milioni 140 ambao wataolewa kabla ya umri wa miaka 18, milioni 50 watakuwa chini ya umri ya 15. "
Na imeripotowa kwamba zaidi ya robo ya wasichana Yemen wanaolewa kabla ya kufikia umri wa miaka 15, na hali hii, si tu hufanya wao kukosa afya na elimu, bibi harusi hao watoto wanakabiliwa na vurugu ya kimwili, kihisia na kijinsia katika ndoa zao za kulazimishwa.
Mwaka 200 sheria Yemen iliunda sheria iliyopitisha umri wa miaka 17 kuwa ndio umri wa msichana kuolewa, lakini bahati mbaya idadi kubwa ya wabunge wa kihafidhina kudai kuwa ni kinyume na uislam.
Jumanne, 20 Agosti 2013
MATUKIO KATIKA PICHA VURUGU ZILIZOTOKEA LEO KATIKA MAANDAMANO YA CHADEMA HUKO JIJINI MWANZA
MAANDAMANO ya amani yaliyokuwa yameandaliwa na chama cha demokrasia na
maendeleo(chadema) yamegeuka shubiri kwa wakazi wa jiji la Mwanza baada
ya kuibuka mapambano makali baina ya waandamanaji hao na jeshi la polisi
mkoani Mwanza na kusababisha polisi kutumia nguvu kuwatawanya wafuasi
wa chama hicho.
Maandamano hayo ya amani ambayo yalianzia katika eneo la Buzuruga nje
kidogo ya jiji la Mwanza yalikuw ayakiongozwa na wabunge Highness Kiwia
wa Ilemela pamoja na Ezekiel Wenje kuelekea katika viwanja vya
Furahisha yalilenga kumshinikiza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Ernest Ndikilo
kutoa barua zinazodaiwa kuandikwa na ofisi ya Waziri Mkuu Tamisemi
kuwarejesha madiwani watatu waliotimuliwa katika Manispaa ya Ilemela
kutokana na kushindwa kuhudhuria vikao vitatu mfululizo.
Polisi wenye silaha pamoja na askari kanzu walianza kutanda katika eneo
hilo la Furahisha wakiongozwa na Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai
Mkoa wa Mwanza RCO Konyo ambaye alikuwa akitumia gari lenye namba za
usajili DK 068EXV aina ya Toyota Land Cruiser
Maandamano hayo ambayo awali yalionekana kana kwamba yangelimalizika
salama yaliwasili katika viwanja vya Furahisha majira ya saa 5.38 huku
yakiongozwa na gari la polisi lenye namba za usajili za nchi ya Uganda
779 UAG likiwa nimesheheni polisi wenye silaha nzito ikiwa ni pamoja na
mabomu ya machozi na bunduki pamoja na askari kadhaa ambao walikuwa
katikati ya maandamano hayo.
Baada ya maandamano hayo kuwasili katika viwanja vya Furahisha kwa
amani,waandamani hao ambao walikuwa na mabango mbalimbali yaliyosomeka
kuwa ‘Matata hatutaki uendelee kuwa Meya wa Ilemela rudia kazi yako ya
awali, na jingine Jaji Sumari tumechoka kuahirisha mara kw amara kesi
dhidi ya Matata na jingine lililosomeka kuwa RD Ndikilo tunahitaji
barua za kurejeshwa kwa madiwani wetu.
Hata hivyo tofauti na ilivyokuwa imetangazwa kuwa maandamano hayo ya
amani yangelipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Ernest Ndikilo,hakukuwa
na kiongozi yoyote wa Serikali ambaye alikuwepo uwanjani hapo kupokea
maandamano hayo.
Kufuatia kutoonekana kwa kiongozi yoyote wa Serikali,viongozi wa chadema
pamoja na wabunge wao walikutana kwa faragha kwa dakika kadhaa kwa
ajili ya kujua hatima ya maandamano hayo ambapo Mbunge wa Nyamagana
Ezekiel Wenje alipanda jukwaani saa 6.45 na kuwaeleza maelfu ya
waandamanaji kuwa wameamua kumtuma Mbunge wa Ilemela Highnes Kiwia
kwenda ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kuchukua majibu kwa ajili ya
kuwaletea wananchi walioandamana juu ya hatima ya madiwani hao.
Hata hivyo saa moja baadae Mbunge huyo alisimama jukwani na wakuwaeleza
waandamani hao kuwa simu ya Mbunge Kiwia ilikuwa haipatikani hivyo
kuwataka kuandamana kwenda kwa Mkuu wa mkoa wa Mwanza kujua kulikoni na
hapo ndipo hali ya hewa ilipochafuka.
Jeshi la polisi baada ya kuona wandamanaji hao wameanza kuelekea katika
ofisi za Mkuu wa mkoa liliwataka kutawanyika ambapo waandamanaji hao
walikaidi ndipo jeshi la polisi lilipoamua kutumia mabomu ya machozi
kuwatawanya wafuasi hao.
Vurugu hizo ambazo zilianza majira ya saa 7.30 zilisababisha kufungwa
kwa baadhi ya barabara kutokana na waandamanji hao kuweka vizuizi vya
mawe na kuchoma matairi,ambapo pia maduka na ofisi mbalimbali
zililazimika kufungwa kwa muda kupisha vurugu hizo.
Baadhi ya wananchi ambao walikuwa wakitumia usafiri wa umma walionekana
wakishuka kupitia katika madirisha ya magari hayo na kukimbia kwa hofu
ya kujeruhiwa na mabomu pamoja na mawe ambayo yalikuwa yakirushwa na
waandamanji hao kwa jeshi la polisi.
MKUU WA MKOA WA MWANZA ALONGA
Mkuu wa mkoa wa Mwanza akizungumza na Mbunge Kiwia pamoja na viongozi wa
chadema ofisini kwake alisema kuwa ameshangazwa na uvumi huo kuwa ofisi
yake imekalia barua a kurejeshwa kwa madiwani Abubakar
Kapera(Nyamanoro),Dan Kahungu(Kirumba) pamoja na Marietha
Chenyenge(Ilemela).
RC Ndikilo alisema kuwa Serikali imekuwa ikifanya kazi zake kwa
maandishi na sio kwa kufuata maneno ya mtaani na kueleza kuwa hana barua
yoyote toka ofisi ya Waziri Mkuu inayomualifu kuhusu kuwarejesha
madiwani hao baada ya kukata rufaa.
“Hata Mbunge kuna siku ulinipigia simu ukiniuliza juu ya kuwepo kwa
barua hizo name nilikujibu kuwa kwa kuwa uko hapo Bungeni Dodoma ambapo
pia kuna ofisi ya Waziri Mkuu nilikujibu kuwa ni muhimu ukawaona
viongozi wakuu wa Tamisemi ikiwa ni pamoja na Waziri Mkuu,pia
nilikushauri kuwa wakupe japo nakala ya barua hiyo”,alisema RC Ndikilo.
“Lakini cha kushangaza nimekuwa nikisikia maneno ya ajabu kuwa nimeficha
barua za madiwani hao,ikumbukwe kuwa madiwnai hao hawakukata rufaa
kwangu bali walikata rufaa ngazi ya juu kabisa,ili kukata mzizi wa
fitina naomba kati ya tarehe 26 hadi 27 wewe Mbunge pamoja na mimi
twende TAMISEMI kukutana na viongozi ili kukata mzizi wa fitina na tuje
tuwaeleze wananchi ukweli uliopo”,alisema RC Ndikilo.
Kuhusu suala la Meya Henry Matata kutoondolewa madarakani RC Ndikilo
alisema kuwa hawezi kulizungumzia suala hilo kw akuheshimu mamlaka ya
mahakama na kuwataka chadema kuvuta subira hadi pale mahakama itakapotoa
maamuzi yake.
KAULI YA MBUNGE KIWIA
Akizungumza katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Kiwia alisema kuwa
waliamua kuitisha maandamano hayo kutokana na kuelezwa na Waziri Hawa
Ghasia kuwa tayari barua hizo zimeishatumwa mkoani Mwanza.
“Mheshimiwa Mkuu wa mkoa hawa madiwani waliosimamishw ani wawakilishi wa
wananchi,wamekaa nje kwa miezi saba sasa na uchaguzi wa Meya haukuwa
halali ndio maana tuliamua kuitisha maandamano kwa ajili ya kuhakikisha
madiwani hawa wanarejeshwa.
RPC MANGU
Akizungumza kwa simu juu ya kutokea kwa vurugu zilizosababisha kupigw
akwa mabomu ya machozi,Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Ernest Mangu
alisema kuwa polisi walifanikiwa kudhibiti vurugu hizo na hadi sasa
hawezi kusema ni wananchi wangapi ambao walikamatwa kuhusu vurugu hizo.
WANANCHI WAWALAUMU VIONGOZI NA WANASIASA NA KUWAPONGEZA POLISI.
Baadhi ya wananchi waliozungumza na Mtanzania juu ya vurugu zilizotokea
waliwaonyoshea kidole wanasiasa pamoja na viongozi wa mkoa wa Mwanza
kutokana na kushindwa kusema ukweli juu ya tukio hilo.
Baadhi walisikika wakisema kuwa kama barua zipo kweli madiwani hao
wanapaswa kupewa na kama azipo basi walioeneza maneno hayo wachukuliwe
hatua kali kutokana na uchochezi.
Wananchi hao pia walilipongeza jeshi la polisi kutokana na kutumia
busara badala ya nguvu kuhakikisha maandamano hayo yanakuwa ya amani.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)