Waumini wakimwombea Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela katika Kanisa la Change Bible katika Mji wa Katlehong uliopo kilometa 40 kutoka Johannesburg jana. Picha na AFP.
Johannesburg, A Kusini Wakati Mandela akiendelea kupatiwa matibabu, mkewe Graca Machel, hajabanduka pembeni mwa kitanda alicholazwa.
Mandela amelazwa katika Hospitali ya magonjwa ya moyo ya Medi-Clinic huko Pretoria tangu Juni 8, mwaka huu na Graca amekuwa akilala hospitali katika chumba kilicho karibu na kile cha Mandela.
Msaidizi wa Mandela, Zelda la Grange alisema, Madiba siku zote amekuwa akitaka Graca awe karibu yake na hata akiumwa hupenda kufahamu yuko sehemu gani.
Hata hivyo, Le Grande, alisema Graca hatumii muda mwingi katika chumba cha hospitali, bali hulala katika kiti kilicho pembeni mwa kitanda cha Mandela.
Wapenzi hao wanatarajiwa kutimiza miaka 15 ya ndoa yao siku tatu kabla ya Mandela kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake ‘Mandela Day’ ambayo kwa Afrika Kusini, siku hiyo ni sikukuu ya kitaifa.
Imeelezwa kwamba Graca ameagiza baadhi ya zawadi, salamu za heshima na pole zinazoletwa hospitali hapo zipelekwe katika Kituo cha Kumbukumbu cha Mandela.
“Machel ameagiza tupeleke zawadi, kadi na barua zinazotumwa kwa ajili ya Mandela katika kituo cha kumbukumbu, pia amesema kama kuna barua au salamu zenye anuani, tujibu. Alishauri hivyo kwa sababu aliona vitu hivyo vikiendelea kukaa nje ya hospitali vitaharibiwa na hali ya hewa” alisema msimamizi wa kituo hicho, Vene Harris.
Tangu Mandela alazwe, Graca amekuwa mkimya, akijitokeza mara chache hadharani kiasi cha kushindwa kukutana na Rais wa Marekani, Barack Obama aliyeitembelea nchi hiyo Julai Mosi.
Wakati watoto na wajukuu wa Mandela wakipigania mabaki ya miili ya watoto watatu wa Mandela wakirushiana maneno makali wakati baba yao yuko mahututi, Graca hajawahi kuzungumza lolote.
Watoto, Serikali wadaiwa kuuza haki ya mazishi
Gazeti la uchunguzi la The Sunday Independent la Afrika Kusini limesema mtoto mkubwa wa Mandela, Makaziwe Mandela na binamu yake, Ndileka wapo kwenye mipango ya kupata fedha kutoka kwa Televisheni ya CNN wakati wa mazishi ya baba yao.
Mmoja wa maofisa wa Shirika la Utangazaji la Afrika Kusini (SABC) ambaye pia alishiriki mkutano huo alikaririwa akisema kwamba Makaziwe na Ndileka walikaa katika mkutano wa siri mwishoni mwa Juni mwaka huu pamoja na maofisa wa shirika hilo na Ofisi ya Rais ili kupanga jinsi ya kuyarusha matangazo ya mazishi ya kiongozi huyo kwa vyombo vya kimataifa
Johannesburg, A Kusini Wakati Mandela akiendelea kupatiwa matibabu, mkewe Graca Machel, hajabanduka pembeni mwa kitanda alicholazwa.
Mandela amelazwa katika Hospitali ya magonjwa ya moyo ya Medi-Clinic huko Pretoria tangu Juni 8, mwaka huu na Graca amekuwa akilala hospitali katika chumba kilicho karibu na kile cha Mandela.
Msaidizi wa Mandela, Zelda la Grange alisema, Madiba siku zote amekuwa akitaka Graca awe karibu yake na hata akiumwa hupenda kufahamu yuko sehemu gani.
Hata hivyo, Le Grande, alisema Graca hatumii muda mwingi katika chumba cha hospitali, bali hulala katika kiti kilicho pembeni mwa kitanda cha Mandela.
Wapenzi hao wanatarajiwa kutimiza miaka 15 ya ndoa yao siku tatu kabla ya Mandela kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake ‘Mandela Day’ ambayo kwa Afrika Kusini, siku hiyo ni sikukuu ya kitaifa.
Imeelezwa kwamba Graca ameagiza baadhi ya zawadi, salamu za heshima na pole zinazoletwa hospitali hapo zipelekwe katika Kituo cha Kumbukumbu cha Mandela.
“Machel ameagiza tupeleke zawadi, kadi na barua zinazotumwa kwa ajili ya Mandela katika kituo cha kumbukumbu, pia amesema kama kuna barua au salamu zenye anuani, tujibu. Alishauri hivyo kwa sababu aliona vitu hivyo vikiendelea kukaa nje ya hospitali vitaharibiwa na hali ya hewa” alisema msimamizi wa kituo hicho, Vene Harris.
Tangu Mandela alazwe, Graca amekuwa mkimya, akijitokeza mara chache hadharani kiasi cha kushindwa kukutana na Rais wa Marekani, Barack Obama aliyeitembelea nchi hiyo Julai Mosi.
Wakati watoto na wajukuu wa Mandela wakipigania mabaki ya miili ya watoto watatu wa Mandela wakirushiana maneno makali wakati baba yao yuko mahututi, Graca hajawahi kuzungumza lolote.
Watoto, Serikali wadaiwa kuuza haki ya mazishi
Gazeti la uchunguzi la The Sunday Independent la Afrika Kusini limesema mtoto mkubwa wa Mandela, Makaziwe Mandela na binamu yake, Ndileka wapo kwenye mipango ya kupata fedha kutoka kwa Televisheni ya CNN wakati wa mazishi ya baba yao.
Mmoja wa maofisa wa Shirika la Utangazaji la Afrika Kusini (SABC) ambaye pia alishiriki mkutano huo alikaririwa akisema kwamba Makaziwe na Ndileka walikaa katika mkutano wa siri mwishoni mwa Juni mwaka huu pamoja na maofisa wa shirika hilo na Ofisi ya Rais ili kupanga jinsi ya kuyarusha matangazo ya mazishi ya kiongozi huyo kwa vyombo vya kimataifa
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni